MAAJABU YA AJALI YA DCM NA ROLI DAR

Ajali ilivyotokea
Na Mwandish wetu, Risasi Jumamosi
DAR ES SALAAM: Wakati ajali mbaya iliyohusisha magari matatu ikiwa bado ndani ya vichwa vya watu jijini Dar es Salaam, baadhi ya mashuhuda wanaelezea maajabu yaliyoambatana na tukio hilo lililotokea Jumatano, likihusisha daladala aina ya Toyota DCM linalofanya safari zake kati ya Gongo la Mboto na Ubungo.
Ajali hiyo ilitokea baada ya daladala yenye namba za usajili T 629 CTT ikiwa na abiria, kugongwa kwa nyuma na lori aina ya Scania lililokuwa limebeba mchanga, lenye namba za usajili T 447 DBH na kuifanya daladala hiyo kupoteza mwelekeo na hivyo kuhama kutoka upande wake hadi wa pili ambako liligongana na Scania lingine lenye namba za usajili T 109 DDX, lililokuwa katika mwendo mkali na kusababisha vifo vya watu wanne na majeruhi 25.
ajaliii (6)
“Nilikuwa ndiyo naingia barabarani ili niende kupanda gari kituoni (Matumbi), nikasikia kishindo kikubwa upande ule wa pili, nilipoangalia vizuri ndipo nikaiona daladala inahamia upande huu, wakati huo lori la ng’ombe nalo lilikuwa linakuja kwa kasi sana. Katika taa kali za gari, nikawaona paka wawili wakiwa katikati ya barabara,” anasema Korongo Japhet, aliyejitambulisha kuwa ni mkazi wa Kigogo Dampo.

Alisema wakati akitafakari kitakachotokea, mara alisikia kishindo kikubwa kilichofuatiwa na kelele nyingi kutoka kwa wasafiri na watu waliokuwa kituoni wakisubiri usafiri.
ajaliii (1)
“Lilikuwa ni tukio la kutisha sana kwa kweli. Sijawahi kukutana na hali hii, mimi huwa mwoga sana, sikusogea eneo la ajali, nikatembea kwa miguu hadi Buguruni ambako nilipanda gari kwenda kibaruani kwangu,” alisema shuhuda huyo.
ajali-(1)
Shuhuda mwingine, Zuwena Boaz mkazi wa Tabata Relini, alisema alikuwa akitembea alfajiri hiyo kuwahi mchicha katika Bonde la Msimbazi wakati aliposikia kishindo kikubwa mara tu baada ya kuingia barabarani.

ajali-(2)
“Mimi nililiona lile DCM likipanda ukuta wa barabara kuhamia upande wa pili, kitu cha ajabu ninachokumbuka kuona ni njiwa wawili weupe wakiruka juu ya ile daladala, lakini sekunde chache baadaye sikuwaona wale ndege, ndipo sasa kikatokea kishindo kingine cha lile lori la ng’ombe, nakumbuka nilikimbia kurudi nilikotoka, nikarudi baadaye nikiwa natetemeka sana,” alisema Zuwena.
ajali
Ajali hiyo ilitokea alfajiri ya Jumatano iliyopita ambapo watu wanne walifariki, watatu eneo la tukio na mmoja alipoteza maisha baada ya kufikishwa katika Hospitali ya Amana, Ilala jijini Dar es Salaam
MAAJABU YA AJALI YA DCM NA ROLI DAR MAAJABU YA AJALI YA DCM NA ROLI DAR Reviewed by The Choice on 11:39:00 PM Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.