Gari linalojiendesha la Google lagonga basi

MOJAWAPO ya gari la Google 
linalojiendesha limegonga basi moja mjini California, Marekani mwezi 
uliopita. Katika ajali hiyo hakuna mtu aliyejeruhiwa.
Sio mara ya kwanza kwa gari 
linalojiendesha la Kampuni ya Google kuhusika katika ajali, lakini 
huenda ni mara ya kwanza kwa magari hayo kufanya ajali.
Kampuni ya Google inatarajia kukutana na
 idara ya magari mjini California ili kuzungumzia kuhusu ajali hiyo na 
kubaini ni nani wa kulaumiwa.

Mnamo Februari 14, mwaka huu gari hilo 
ambalo lilikuwa likisafiri kwa kasi ya kilomita 3 kwa saa liligonga basi
 moja la umma lililokuwa likisafiri kwa kasi ya kilomita 24 kwa saa.
Mtu aliyekuwa katika gari hilo la Google
 aliripoti kwamba alidhani basi hilo lingepunguza mwendo ili kuisubiri 
gari hiyo kupita hivyo basi hakuingilia kompyuta inayoendesha gari hilo.
Ajali hiyo ilitokea katika eneo la Mountain View karibu na makao makuu ya Kampuni ya Google.
Katika taarifa yake Google ilisema “Tunabeba lawama kwa sababu iwapo gari letu lisingeenda kusingekuwa na ajali
Gari linalojiendesha la Google lagonga basi
![Gari linalojiendesha la Google lagonga basi]() Reviewed by The Choice
        on 
        
10:09:00 PM
 
        Rating:
 
        Reviewed by The Choice
        on 
        
10:09:00 PM
 
        Rating: 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
No comments: